Maelezo ya Chini
a Huenda ile “sauti tulivu, ya chini” ilikuwa ya malaika aliyetumiwa kupeleka “neno la Yehova” anayetajwa katika 1 Wafalme 19:9. Katika mstari wa 15 malaika huyo anatajwa kama “Yehova.” Huenda tukakumbuka mjumbe wa Yehova aliyetumiwa kuwaongoza Waisraeli nyikani na ambaye Mungu alisema hivi kumhusu: “Jina langu limo ndani yake.” (Kut. 23:21) Bila shaka, hatuwezi kusema jambo hili kwa uhakika, lakini tunapaswa kukumbuka kwamba kabla ya kuja duniani, Yesu alikuwa “Neno,” Msemaji maalumu wa Yehova kwa watumishi wake.—Yoh. 1:1.