Maelezo ya Chini
a Ni muhimu kujua kwamba Yona alitoka Galilaya kwa sababu Mafarisayo walisema hivi kwa kiburi kumhusu Yesu: “Chunguza uone kwamba hakuna nabii atakayeinuliwa kutoka Galilaya.” (Yoh. 7:52) Watafsiri na watafiti wengi wamedokeza kuwa Mafarisayo walisema kwa ujumla kwamba hakuna nabii aliyetoka wala ambaye angetoka eneo la hali ya chini la Galilaya. Ikiwa ndivyo, walikuwa wakipuuza historia na pia unabii.—Isa. 9:1, 2.