Maelezo ya Chini
a Mfalme aliwaruhusu Wayahudi waendelee kupigana na adui zao siku iliyofuata ili wawashinde kabisa. (Esta 9:12-14) Mpaka leo, Wayahudi husherehekea ushindi huo kila mwaka katika mwezi wa Adari, ambao unalingana na mwishoni mwa Februari na mwanzoni mwa Machi. Sherehe hiyo inaitwa Purimu, na ilipata jina kutokana na kura ambayo Hamani alipiga alipokuwa akipanga kuwaangamiza Waisraeli.