Maelezo ya Chini
c Jambo moja lililopunguza uzito wa maonyo hayo ni kwamba yalihusu hasa kundi dogo la Kristo la watu 144,000. Katika Sura ya 5 tutaona kwamba kabla ya mwaka wa 1935, ilidhaniwa kuwa “mkutano mkubwa” unaotajwa kwenye Ufunuo 7:9, 10 katika tafsiri ya Union Version, ungetia ndani washiriki wengi wa makanisa ya dini zinazodai kuwa za Kikristo na kwamba washiriki hao wangekuwa kundi la pili lenye tumaini la kwenda mbinguni, hiyo ikiwa thawabu yao kwa kumuunga mkono Kristo hadi kuja kwake.