Maelezo ya Chini
b Kijitabu To Whom the Work Is Entrusted (Kwa Wale Waliokabidhiwa Kazi) kilieleza hivi: “Gazeti The Golden Age litatumiwa katika kampeni ya kupeleka ujumbe wa ufalme nyumba kwa nyumba. . . . baada ya kutoa ujumbe huo, nakala ya The Golden Age inapaswa kuachwa katika kila nyumba, iwe mtu ameandikisha gazeti hilo au la.” Kwa miaka mingi baada ya hapo, akina ndugu walitiwa moyo wawatolee watu maandikisho ya The Golden Age na Mnara wa Mlinzi. Kuanzia Februari 1, 1940, watu wa Yehova walitiwa moyo wawaachie watu magazeti hayo na waripoti magazeti waliyowaachia watu.