Maelezo ya Chini
d Yesu alifundisha jambo hilohilo katika mfano wake kuhusu mwanabiashara anayesafiri kutafuta lulu moja ya thamani kubwa. Anapoipata, mwanabiashara huyo anauza vitu vyote alivyo navyo na kuinunua. (Mt. 13:45, 46) Pia, mifano yote miwili inatufundisha kwamba tunaweza kujifunza kweli ya Ufalme katika njia mbalimbali. Wengine hupata kweli hiyo bila kutarajia; hali wengine huitafuta. Lakini hata iwe tulipata kweli kwa njia gani, tuko tayari kujidhabihu ili tuutangulize Ufalme maishani.