Maelezo ya Chini
a Wayahudi kutoka maeneo mengine waliokuja hekaluni walipaswa kulipia kodi ya hekalu ya kila mwaka kwa kutumia aina fulani ya sarafu, na wale waliobadili pesa waliwatoza malipo fulani ili kuwabadilishia sarafu hizo. Kwa kuongezea, huenda wageni hao walihitaji kununua wanyama kwa ajili ya kutoa dhabihu. Yesu aliwaita wafanyabiashara hao “wanyang’anyi,” labda kwa sababu walitoza malipo ya juu kupita kiasi kwa ajili ya huduma zao.