Maelezo ya Chini
c Injili ya Luka inaorodhesha majaribu hayo kwa mpangilio tofauti, lakini inaonekana simulizi la Mathayo linataja jinsi matukio hayo yalivyofuatana. Chunguza sababu tatu. (1) Mathayo anaanza kutaja jaribu la pili kwa neno “ndipo,” kuonyesha kwamba ndilo tukio lililofuata. (2) Inapatana na akili kuamini kwamba majaribu mawili yaliyotungwa kwa ujanja—kila moja likianza kwa maneno, “Ikiwa wewe ni mwana wa Mungu”—yangefuatwa na jaribu la waziwazi la kuvunja amri ya kwanza. (Kut. 20:2, 3) (3) Maneno ya Yesu “Nenda zako, Shetani!” kwa kweli yangefuata jaribu la tatu na la mwisho.—Mt. 4:5, 10, 11.