Maelezo ya Chini
b Neno “wivu” linaonyesha jinsi Yehova anavyothamini uaminifu. Tunaweza kufikiria jinsi mume anavyokasirika na kuwa na wivu ikiwa mke wake anakosa kuwa mwaminifu. (Met. 6:34) Kama mume huyo, Yehova alikasirika Waisraeli walipokosa kuwa waaminifu kwa kuabudu sanamu. Kitabu kimoja cha marejeo kinasema: “Wivu wa Mungu . . . unachochewa na utakatifu wake. Kwa kuwa yeye peke yake ndiye mtakatifu . . . , Hakubali ibada nyingine.”—Kut. 34:14.