Maelezo ya Chini
b Baadhi ya wasomi wanaelewa kwamba maneno haya yanatoa wazo zuri, wanasema kwamba kuvuna chumvi ili kuitumia kuhifadhi vitu ni biashara ya muda mrefu yenye faida katika eneo la Bahari ya Chumvi. Hata hivyo, ona kwamba simulizi hilo lilisema waziwazi kwamba sehemu hizo zenye matope “hazitaponywa.” Zinabaki bila uhai, bila kuponywa, kwa sababu maji yanayoleta uhai kutoka katika nyumba ya Yehova hayafiki huko. Basi inaonekana kwamba katika simulizi hili chumvi ya maeneo hayo yenye matope inatajwa kwa njia isiyo nzuri.—Zab. 107:33, 34; Yer. 17:6.