Maelezo ya Chini
b Vitabu vingi vya maelezo ya Biblia, vinapozungumza 1 Timotheo 5:20, vinatoa maelezo kupatana na jambo hilo. Kile cha Albert Barnes chasema: “. . . maana hapa inahusiana na vile mkosaji ambaye amehakikishwa kuwa ana hatia anavyopaswa kutendewa, na ikiwa jambo lile limejulikana na hadhara ya watu. Halafu inapaswa ionyeshwe hadharani kwamba jambo hilo limelaumiwa.” Kitabu cha maelezo cha Schaff-Lange kinasema: “Namna ya kisa chenyewe yahitaji kwamba neno ha·mar·taʹnon·tas lifahamike hasa kutumiwa juu ya uhalifu mbaya zaidi; ule unaoleta kashifa.” Henry’s Bible Commentary yasema: “Watenda dhambi wa hadhara, wenye kukashifu lazima wakemewe hadharani; kwa maana dhambi yao wameitenda hadharani, mbele ya watu wengi, au habari zake zikasikiwa na wote, kwa hiyo lazima karipio lao liwe hadharani, na mbele ya wote.”