Maelezo ya Chini
b Kama vitabu vinavyoonyesha, Kanisa Katoliki mwishowe lilijidai kuwa na haki ya pekee ya kuweka sheria zinazohusu ndoa, likatokeza sheria na vizuizi vyake lenyewe na kushikilia kwamba lazima wakuu wa serikali waongozwe na sheria hizo. Waprotestanti wenye kufanya Matengenezo ya kanisa walikuwa tofauti sana wakaachia wakuu wa serikali waamue karibu mambo yote yaliyohusu ndoa. Katika Uingereza, Scotland na Ireland sherehe ya kiserikali ilianzwa mwaka 1653 ili kukomboa Kanisa na mambo ya kilimwengu. Sheria ya Kifaransa ya 1792 ilifanya iwe lazima sherehe ya kiserikali ifuatwe na raia wote kwa kutegemea kanuni ya kwamba “raia ni mali ya Serikali, hata awe wa dini gani.” (The New Schaff-Herzog Religious Encyclopedia, Vol. VII, kur. 199, 200)