Maelezo ya Chini
a Ezekieli 31:3, NW, unasema katika sehemu moja hivi: “Tazama, Mwashuru, mwerezi katika Lebanoni.” Inafaa ionwe kwamba tafsiri nyingine (UV, ZSB, n.k.) hapa zinasomwa hivi: “Tazama Mwashuru alikuwa mwerezi katika Lebanoni . . . ” Hili lilikuwa limefanya lieleweke kwamba “mti” huo mkubwa ulifananisha Ashuru wa kale. Lakini neno hili “alikuwa” halionekani katika maandishi ya Kiebrania ya kale. Na habari inayozunguka neno hilo inaonyesha kwamba onyo hilo lilitolewa kwa Farao na wingi wa watu wake, anayetajwa akifanana na “Mwashuru” na vile vile akifanana na “mwerezi katika Lebanoni.” Kwa wazi basi “Mwashuru” anatajwa tu ili kuonyesha wazo la uwezo mkubwa wa kijeshi, na hivyo ndivyo ilivyokuwa Misri ya kale.