Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO

Maelezo ya Chini

a Maneno ya mtume katika Warumi 1:24-27 yametajwa juu ya “matumizi ya asili” ya miili ya kiume na ya kike. Kama inavyoonekana wazi na kama vile imekubaliwa kwa kupatana, maneno hayo yanahusu hali ya kulalana wanaume kwa wanaume na wanawake kwa wanawake. Hayahusu moja kwa moja ngono zinazofanywa kati ya mume na mke hata kidogo. Inapaswa kukubaliwa vilevile kwamba hata mahaba (mapenzi) ambalo ni jambo la kawaida kabisa linalofanywa kati ya mume na mke, yangekuwa “yasiyo ya asili” yakifanywa kati ya wanaume kwa wanaume au wanawake kwa wanawake. Tena lingekuwa tendo la ufisadi ikiwa lingefanywa na watu wasiofunga ndoa. Kwa hiyo, uongozi wo wote unaotolewa na maneno hayo ya mtume, hauhusu moja kwa moja ngono zinazofanywa katika mpango wa ndoa. Lakini unapaswa uonwe kuwa wa namna ya kushawishi tu, si wa namna ya kukata maneno, yaani, sio msingi wa kuwekea kanuni za uamuzi ambazo hazina sababu nzuri. Lakini inaweza kuwa kwamba labda mwanzoni ngono nyingine zinazofanywa wakati huu na mume na mke zilifanywa kati ya wanaume kwa wanaume na wanawake kwa wanawake tu. Ikiwa ingekuwa hivyo, basi mwanzo wa mazoea hayo ungekuwa si mzuri kabisa. Kwa hiyo, kwa sababu maneno hayo yaliyo katika maandiko yaliyotangulia kutajwa hayahusu moja kwa moja watu waliofunga ndoa. Mkristo aliye na dhamiri asipuze jambo hilo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki