Maelezo ya Chini
a Maana yake, mtu huyo angekuwa akiwaambia wazazi wake hivi: ‘Kwa habari yenu, mali yangu ni “Korbani,” zawadi iliyowekwa wakf kwa Mungu, na hamwezi kuitumia au kujifaidi nayo kwa vyo vyote.’ Kwa kutumia neno “Korbani,” haina maana kwamba mtu alikuwa akiweka mali yake wakf kwa Mungu. Kwa kawaida neno hilo lilimaanisha kwamba alikuwa tu akiifanya kuwa kama zawadi iliyowekwa wakf kwa Mungu, ili kwamba mtu au watu aliosema nao wasiweze kuitumia. Katika kitabu The Life and Times of Jesus the Messiah (Maisha na Nyakati za Yesu, Masihi), Alfred Edersheim anaandika hivi: “Haiwezi kupingwa kwamba nadhiri za namna hiyo, kuhusiana na wazazi, zingefuatwa, na kwamba kwa kweli zilitolewa.”