Maelezo ya Chini
b Yesu alitumia mtajo “wa imani haba” kwa habari ya wanafunzi wake peke yao. Unaonekana pia katika Mathayo 8:26; 14:31; 16:8 na Luka 12:28. Kifungu hicho cha maneno kinapatikana katika maandishi ya kirabi, jambo hilo likionyeshwa kwamba ulikuwa ukifahamika vizuri. Kwa mfano, kitabu Babylonian Talmud kinasimulia hivi: “R[abi] Eliezeri mkuu atangaza hivi: Ye yote aliye na kipande cha mkate katika kikapu chake naye asema, ‘Nitakula nini kesho?’ Ni mmoja wa wale wa imani haba”