Maelezo ya Chini
a Jina “Asafu” linapatikana katika maandishi ya juu ya Zaburi 50 pamoja na Zaburi 73 mpaka 83 katika tafsiri ya New World. Kwa kuwa Zaburi 79 na 80 hutaja matukio yaliyotukia baada ya wakati wa mwanamuziki Mlawi Asafu, nyingine za zaburi hizi lazima ziwe ziliandikwa na wazao wake. Kwa hiyo, kwa wazi jina “Asafu” lazima lifahamike kuwa linatia ndani nasaba yote ya wazao wake iliyoanza naye. Kwa kuwa hakuna jambo lo lote katika yaliyomo Zaburi 73 linaloonyesha kwamba iliandikwa katika wakati wa baadaye, tunaweza kuamua kwamba iliandikwa na mwanamuziki Mlawi mwenyewe, aliyeishi wakati ule ule na Mfalme Daudi.