Maelezo ya Chini
a Alipokuwa akizungumza na mitume wake 12 wakati wa Chakula cha Jioni cha mwisho, Yesu alitumia maneno haya ya Daudi. Akionyesha uhakika wa kwamba mmoja wa wale 12 angemsaliti, Yesu alisema hivi: “Nawajua wale niliochagua. Walakini kusudi ni kwamba Andiko litimizwe, ‘Yeye aliyekuwa akila mkate wangu ameinua kisigino chake juu yangu.’” (Yohana 13:18, NW) Mungu alikuwa anajua kwamba Yesu angetendewa vibaya na mshiriki wa karibu katika njia ambayo ilifanana na yale yaliyompata Daudi.