Maelezo ya Chini
a Hiyo inafanana na vile alivyosema Yesu katika mfano wake wa ngano na magugu, kwamba “shamba” lilikuwa ulimwengu wa watu. (Mt. 13:38) Ila hapa, katika Marko 4:26-29, “nchi” ambayo ndani yake mbegu zinapandwa, badala ya kuwa ulimwenguni pote, inahusu tu watu ambao mtu mmoja mmoja anakutana nao na kushirikiana nao. “Nchi” haifananishi “moyo” wa watu mmoja mmoja, kama vile katika Mathayo 13:19 na Luka 8:12, 15.