Maelezo ya Chini
b Kupatana na fundisho hili la Biblia, Adam Clarke anaikazia tofauti, akisema: “Msifanye mashauriano pamoja na [mtenda dhambi aliyeondoshwa nje] katika mambo matakatifu wala ya kiraia. Mnaweza kuendesha shughuli zenu za kilimwengu pamoja na mtu asiyemjua Mungu, asiyesema ni Mkristo, hata awe ana tabia ya adili ya namna gani; lakini, haiwapasi kamwe mfikie kiasi hicho cha kutambua mtu mwenye kusema ni Mkristo, anayefuata mwenendo wenye kuleta aibu. Mwacheni huyo atiwe alama hii ya ziada ya kuchukia kwenu dhambi ya namna zote kiasi cha kutapika.’’