Maelezo ya Chini
b Hakuna maandishi yanayoonyesha wanafunzi hao wa kwanza wa Yesu walibatizwa tena kuwa mfano wa kujitoa kwao wakati fulani kabla ya roho takatifu kumwagwa juu yao katika Pentekoste. Kwa wazi ubatizo wao wa kwanza wa toba walipokuwa wangali chini ya Torati ulitia ndani jambo hilo, nalo hilo lingekuwa ni kumwiga Yesu, kwa kuwa ubatizo wa Yohana ulifanywa kwa kutarajia kutokea kwa Masihi nao uliwatayarisha kwa ajili ya mapenzi ya Mungu kwao kuhusiana na kuja kwake.