Maelezo ya Chini
a Wale wanaofufuliwa kwenye “ufufuo wa uzima” au kwenye “ufufuo wa hukumu” hawapaswi kuonwa ni wale wale sawa na “wenye haki” na “wasio haki” wanaotajwa na Paulo katika Matendo 24:15. Paulo anazungumza juu ya hali ya watu wakati wanapofufuliwa, ikitegemea mwenendo wao kabla ya kufa. “Wenye haki” watapaswa kuendelea na mwendo wao wa kutenda kwa kutii mambo yaliyoandikwa katika vile “vitabu.” Kama sivyo ufufuo wao ungeweza kugeuka uwe “wa hukumu.” Vivyo hivyo, watu wo wote “wasio haki” wakitubu, wakikubali dhabihu ya ukombozi ya Kristo na kutii mambo yaliyoandikwa katika “vitabu” hivyo, ufufuo wao ungeweza kuwa “wa uzima.”