Maelezo ya Chini
a Hali inayotokea mara chache na inayohuzunisha ni ile ya msichana mchanga anayezaa mtoto baada ya kulalwa kinguvu. Wale wanaohusika hasa, msichana huyo na wazazi wake, wanaweza kuamua mwendo wa hekima ni nini kuhusiana na mambo yote yaliyopo, kutia hali ya kimwili na ya moyoni ya msichana huyo. Katika visa vingine kama hicho kitoto kimekubaliwa na kulelewa kwa upendo kwa njia ya Kikristo katika jamaa ya msichana huyo. Katika visa vingine wenzi wengine Wakristo wanaotaka kutunza mtoto, na wakiweza kufanya hivyo, wameruhusiwa kumlea mtoto huyo.