Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO

Maelezo ya Chini

b Inastahili kuangaliwa kwamba kamusi Webster’s New Collegiate Dictionary inatanguliza maelezo yafuatayo kuwa ndiyo maana ya neno “uasherati”: “Ngono ya kibinadamu iliyo tofauti na ile inayofanywa kati ya mwanamume na mke wake.” Na katika kueleza maana ya “ngono” (kati ya mwanamume na mwana mke, ya kutumia mkundu, ya kutumia mdomo), kamusi hiyo inataja kwamba tendo linakuwa ngono linapohusu “kiungo cha uzazi cha angaa mtu mmoja.” Kwa hiyo neno la Kiingereza “fornication” (uasherati) ni tafsiri inayofaa ya neno la Kigiriki porneia.

Kwa mfano, The New International Dictionary of New Testament Theology inasema kwamba porneia ni neno lenye maana ya “unajisi, ukahaba, umalaya uasherati.” Inasema hivi pia: “Fungu la maneno yenye maana zinazokaribiana [linalohusu porneia] linaweza kumaanisha namna mbalimbali za ngono zinazofanywa nje ya ndoa kwa kuwa hazifuati kawaida zinazokubaliwa kijamii na kidini (kwa mfano, kulalana kwa watu wa jinsi moja, kufanya ngono na mtu ye yote tu bila kujali, kuwatumia watoto isivyopasa kwa kufanya ngono nao, na hasa umalaya).” Hivyo, neno porneia lingetia ndani uzinzi (Kigiriki, moikheia), na linaweza kuhusu namna nyingi zaidi za mazoea ya ufisadi yanayofanywa nje ya ndoa, kama vile kufanya ngono ya kuingiza uume ndani ya mdomo au mkundu wa mwingine na kulalana na mnyama.

Chapa ya mwaka wa 1979 ya ile kamusi inayoheshimiwa sana inayoitwa Greek-English Lexicon of the New Testament and Other Early Christian Literature (iliyotayarishwa na Bauer, Arndt na Gingrich) inaeleza maana ya porneia kuwa “umalaya, unajisi, uasherati wa kila namna ya ngono zilizo haramu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki