Maelezo ya Chini
a Tafsiri fulani za Biblia zinasema, “Huu ndio mwili wangu.” (Ona Union Version, Habari Njema kwa Watu Wote, na Zaire Swahili Bible.) Lakini, neno la Kigiriki lililotumiwa kuwa “ndio” au “ni” ni neno e·stin, kuonyesha kufananisha, kumaanisha, kuwakilisha. (Ona maneno ya chini juu ya Mathayo 26:26, NW Biblia ya uchunguzi.) Neno ilo hilo la Kigiriki linaonekana katika Mathayo 9:13 na 12:7 na katika visa vyote viwili linatafsiriwa kuwa “maana” (UV, ZSB, na HNWW).