Maelezo ya Chini
a Mambo ya kisiasa leo yako tofauti sana na vile yalivyokuwa siku za Yohana. Ni mataifa machache sana yaliyo washirika wa Umoja wa Mataifa yaliyokuwa yametokea wakati huo. Kwa hiyo, ni jambo la kweli kusema kwamba walikuwa “hawajapokea ufalme bado.” Ni machache tu yaliyokuwako, kama Misri. Lakini hata katika nchi hizo, hali ya mamlaka imebadilika sana muda wa karne zilizopita hivi kwamba maelezo ya malaika yule yangali ya kweli: Serikali zilizo na mamlaka sasa zilikuwa ‘hazijapokea ufalme bado’ katika siku za Yohana.