Maelezo ya Chini
b Wakati Vita ya Ulimwengu ya Pili ilipokuwa ikiendelea kuwaka kweli kweli, msimamizi wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi alitoa hotuba yenye kichwa “Amani—Je! Inaweza Kudumu?” akihutubia Ulimwengu Mpya wa Kitheokrasi Mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova siku ya Septemba 20, 1942. Humo, alionyesha kutokana na Ufunuo sura ya 17 kwamba, tofauti na vile wengi walivyotazamia, Vita ya Ulimwengu ya Pili haingekuwa Har–Magedoni mwishowe bali kwamba ni lazima kwanza yule ‘mnyama wa amani’ atokea tena kutoka lile shimo refu sana la kutokutenda ili atawale muda wa “saa moja” ya mfano pamoja na mamlaka za kisiasa.”