Maelezo ya Chini
b Katika kichapo chao Commentary on the Old Testament, Keil na Delitzsch wanasema kwamba mtu angekuwa mwenye hatia ya kosa au dhambi ikiwa ‘alijua uhalifu wa mwingine, awe alikuwa ameuona, au alikuwa amekuja kuujua kwa uhakika kwa njia nyingine yo yote, na hivyo akastahili kuonekana mahakamani akiwa shahidi wa kushtakiwa kwa mhalifu, lakini hakujali kufanya hivyo, na hakusema jambo alilokuwa ameona au kujua, wakati alipokisikia kiapisho kizito cha mwamuzi kwenye uchunguzi wa hadharani juu ya uhalifu ule, ambao kupitia huo watu wote waliopo, waliojua habari yo yote juu ya jambo hilo, walihimizwa wajitokeze kuwa mashahidi.”