Maelezo ya Chini
a Sheria ya Hammurabi haikuwa na maandalizi kama hayo; wala fungu la sheria za usafi wa kiafya linalolingana na hilo halijavumbuliwa miongoni mwa Wamisri wa kale, ingawa wao walitumia namna ya hali ya juu ya dawa kwa kulinganisha. Kinasema kitabu Ancient Egypt: “Maneno na maelezo ya michanganyiko ya kiuganga yanachanganywa pamoja bila kizuizi [katika vitabu vya dawa vya Wamisri] na hati zilizoandikwa zinazopatana na akili.” Sheria ya Mungu, hata hivyo, haikuwa na madokezo yo yote ya kishetani lakini ilikuwa sahihi kisayansi. Ni katika nyakati za ki-siku-hizi, kwa mfano, kwamba madaktari wameona uhitaji wa kujiosha baada ya kugusa maiti, jambo ambalo Sheria ya Musa ilitaka mileani nyingi zilizopita!—Hesabu sura 19.