Maelezo ya Chini
a Yohana alitumia khai’ro hapa, ambayo ilikuwa salamu kama “uwe na siku njema” au “jambo.” (Matendo 15:23; Mathayo 28:9) Yeye hakutumia a·spaʹzo·mai (kama katika mstari 13), neno ambalo linamaanisha “kuzungushia kwa kushika katika mikono, hivyo kusalimu, kukaribisha” na huenda likawa liligusia maana ya salamu ya uchangamfu sana, hata pamoja na kumbatio. (Luka 10:4; 11:43; Matendo 20:1, 37; 1 Wathesalonike 5:26) Kwa hiyo mwelekezo ulio kwenye 2 Yohana 11 ungeweza pia kumaanisha kutosema hata “jambo” kwa watu hao.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Januari 15, 1986, ukurasa 30.