Maelezo ya Chini
b Franz von Papen alikuwa miongoni mwa Wanazi waliojaribiwa kama wahalifu wa vita kule Nuremberg, Ujeremani, katika miaka ya mwishoni mwa 1940. Yeye aliwekwa huru na hatia lakini baadaye akapata hukumu kali kutoka mahakama moja ya Ujeremani yenye kushughulikia mabaya yaliyotendwa na chama cha Nazi. Na bado baadaye, katika 1959, alifanywa Chambaleni wa Baraza la Faragha la Papa.