Maelezo ya Chini
a Wanafunzi wengi wa Biblia wang’amua kwamba nadharia hii ni yenye kosa kwa kuwa Maandiko ya Kigiriki, yaliyoandikwa katika karne ya kwanza W.K., yana kumbukumbu la maandishi ya utimizo wa unabii mwingi wa Maandiko ya Kiebrania ambayo yaweza kuthibitishwa kwamba yaliandikwa karne kadhaa mapema. Kwa kielelezo, utimizo wa karne ya kwanza wa maelezo yote ya Danieli 9:24-27 umeandikwa ama katika Maandiko ya Kigiriki ama na wanahistoria wa mambo ya kilimwengu.