Maelezo ya Chini
a Huko Masada, waakiolojia walipata mamia ya sarafu zenye miandiko ya Kiebrania zikiadhimisha uasi huo, kama vile “Kwa ajili ya uhuru wa Sayuni” na “Yerusalemu Takatifu.” Dakt. Yigael Yadin katika kitabu chake Masada aeleza hivi: “Shekeli tulizopata zawakilisha miaka yote ya uasi, kuanzia mwaka wa kwanza hadi ule mwaka wa tano wa shida, mwaka wa mwisho ambapo shekeli hiyo iliundwa, ukilingana na mwaka 70 AD ambapo Hekalu la Yerusalemu liliharibiwa.” Angalia sarafu iliyo juu.