Maelezo ya Chini
a Miongoni mwa mambo mengine, makala hii ilisema hivi: “Hakujapata kamwe kuwa na ushahidi mpana sana wa ukweli kama katika miaka michache iliyopita. . . . Mabaki wanawaletea ujumbe wenye kufurahisha, na wanawaambia hivi: ‘Na yeyote anayetaka, acheni atwae maji ya uhai bure.’ Wao wanaambiwa kwamba sasa wanaweza kuchukua msimamo wao upande wa Bwana, na dhidi ya Ibilisi, na kupokea baraka. Je! jamii ya watu wa jinsi hiyo siyo inayoweza sasa kutafuta usikivu na uadilifu, na kufichwa katika siku ya hasira kuu yake itakayoonyeshwa, na kupelekwa ng’ambo ya lile pigano kubwa la Har–Magedoni na kuishi milele isife? (Sef. 2:3) . . . Jamii yenye uaminifu ya mabaki inajiunga katika mwaliko huo wenye neema na kusema, ‘Njoo.’ Ujumbe huu unapasa kupigiwa mbiu kwa wale walio na tamaa ya uadilifu na ukweli. Ni lazima ifanyike hivyo sasa.”