Maelezo ya Chini
b Mnara wa Mlinzi la Agosti 15, 1934 (Kiingereza), lilitaja pia daraka la kondoo wengine na kusema hivi katika ukurasa wa 249, fungu la 31: “Jamii ya Yonadabu ni wale ambao ‘wanasikia’ ujumbe wa ukweli na ambao ni lazima waseme hivi kwa wale wanaowasikia: ‘Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure.’ (Ufu. 22:17) Wale wa jamii ya Yonadabu ni lazima waambatane na wale walio wa shirika la Yehu mfananishwa, yaani, wapakwa-mafuta, na watangaze ujumbe wa ufalme, hata ingawa wao si mashahidi wapakwa-mafuta wa Yehova.”