Maelezo ya Chini
a Linganisha njia mbili ambazo kwazo Paulo aliitikia juu ya swala la tohara. Ingawa alijua kwamba “kutahiriwa si kitu,” yeye alimtahiri Timotheo mwandamani wake wa kusafiri, aliyekuwa Myahudi kwa upande wa mama yake. (1 Wakorintho 7:19; Matendo 16:3) Katika kisa cha Tito, mtume Paulo aliepuka kumtahiri likiwa jambo la kikanuni katika shindano pamoja na Watetezi wa Dini ya Kiyahudi. (Wagalatia 2:3) Tito alikuwa Mgiriki na kwa hiyo, tofauti na Timotheo, yeye hakuwa na sababu yoyote halali ya kutahiriwa. Ikiwa yeye, mtu Asiye Myahudi, angetakiwa atahiriwe, ‘Kristo hangemfaidia neno.’—Wagalatia 5:2-4.