Maelezo ya Chini
a Wote wawili Yesu na Yakobo husema kwamba haikunya mvua katika nchi kwa “miaka mitatu na miezi sita.” Hata hivyo, yasemekana kwamba Eliya alijitokeza mbele ya Ahabu mwishoni mwa ukame “katika mwaka wa tatu”—bila shaka kuhesabu tokea siku ile alipotangaza ukame. Hivyo, lazime iwe ilikuwa mwishoni mwa majira marefu ya ukame, usiyo na mvua wakati aliposimama mbele ya Ahabu kwa mara ya kwanza.—Luka 4:25; Yakobo 5:17; 1 Wafalme 18:1.