Maelezo ya Chini
b Baada ya kusali sana na kulichunguza sana Neno la Mungu, Joseph Rutherford aliona wazi jibu alilopaswa kuwapa ndugu katika Ujerumani. Halikuwa jukumu lake kuwaambia la kufanya na lisilo la kufanya. Wao walikuwa na Neno la Mungu, lililowaambia kwa wazi wapaswayo kufanya kwa habari ya kukutana pamoja na kutoa ushahidi. Kwa hiyo akina ndugu Wajerumani walianza kufanya kazi kichinichini lakini waliendelea kutii amri za Yehova za kukutana pamoja na kutoa ushahidi wa jina lake na Ufalme wake.