Maelezo ya Chini
b Waisraeli walifahamu ule utaratibu wa kuyeyusha. Masalio yamepatikana ya baadhi ya migodi ya shaba nyekundu, na shaba nyekundu iliyeyushwa ili kutayarisha vyombo vya hekalu. (Linganisha 1 Wafalme 7:14-46.) Yaonekana kwamba utaratibu huo wa kuyeyusha usingaliweza kufanywa bila kutokeza kadiri fulani ya uchafuzi kwa namna ya mioshi, mavi ya madini, na povu, kukiwa pia na athari nyinginezo. Hata hivyo, yaonekana Yehova alikuwa na nia ya kuvumilia kadiri ndogo ya uchafu wa mahali fulani katika mkoa huo usio na wakaaji wengi na ulio mbali.