Maelezo ya Chini
a Kule kuteseka kwingi ambako Yesu alivumilia kwaweza labda kuonwa kutokana na jambo la kwamba mwili wake mkamilifu ulikufa baada ya muda wa saa chache tu ukiwa mtini, ilihali wale watenda maovu waliotundikwa kando yake walilazimika kuvunjwa miguu ili kuharakisha kifo. (Yohana 19:31-33) Hawakuwa wamepatwa na kule kuteseka kiakili na kimwili kulikompata Yesu katika lile jaribu la usiku kucha bila usingizi kabla ya kutundikwa, labda kufikia hatua ambayo hangeweza hata kuchukua mti wake mwenyewe wa mateso.—Marko 15:15, 21.