Maelezo ya Chini
f Profesa Walter L. Liefeld aandika hivi: “Kwa hakika yawezekana kuona kwamba tabiri za Yesu zilitia ndani sehemu mbili: (1) matukio ya A.D. 70 yaliyohusisha hekalu na (2) yale ya muda mrefu baadaye katika wakati ujao, yanayoelezwa katika maneno ya kiapokalipsi [ufunuo] zaidi.” Ufafanuzi uliohaririwa na J. R. Dummelow wasema hivi: “Mengi ya magumu mazito zaidi ya hotuba hiyo kuu hutoweka inapong’amuliwa kwamba Bwana yetu hakurejezea ndani yayo tukio moja bali mawili, na kwamba lile la kwanza lilifananisha lile la pili. . . . [Luka] 21:24 hasa, linalosema juu ya ‘nyakati za Wasio Wayahudi,’ . . . laweka kipindi cha katikati kisicho dhahiri kati ya anguko la Yerusalemu na mwisho wa ulimwengu.”