Maelezo ya Chini
c Yosefo aandika juu ya matukio kati ya shambulio la kwanza la jeshi la Waroma dhidi ya Yerusalemu (66 W.K.) na kuharibiwa kwalo: “Wakati wa usiku dhoruba yenye uharibifu mkubwa ilitokea; kimbunga kilipiga, mvua kubwa ajabu ilinyesha, umeme ulizidi kumweka, ngurumo zilikuwa zenye kuogofya, dunia ilitetemeka kwa mingurumo yenye kutia uziwi. Msiba kwa jamii ya kibinadamu ulitangulia kufananishwa waziwazi na mvunjiko huo wa muundo mzima wa mambo, na hakuna mtu angeweza kutia shaka kwamba ishara hizo zilimaanisha balaa isiyo na kifani.”