Maelezo ya Chini
a Watu wengi bado huwaendea shamani, wachawi, au waponyaji kama hao. Shamani ni “kuhani anayetumia uchawi kwa kutibu wagonjwa, kufunua yaliyofichwa, na kudhibiti matukio.” Mchawi au shamani, aweza kuchanganya majani na mambo ya kiuchawi (akiomba nguvu za kifumbo). Mkristo mwangalifu aliye mwaminifu-mshikamanifu angeepuka kujiingiza katika mambo ya uwasiliani-roho kama hayo, hata kama yaonekana atatibiwa.—2 Wakorintho 2:11; Ufunuo 2:24; 21:8; 22:15.