Maelezo ya Chini
a Kwa kweli, wao waliwapuuza maskini kwa kutumia ule mtajo “ʽam-ha·ʼaʹrets,” au “watu wa ardhi.” Kulingana na msomi mmoja, Mafarisayo walifundisha kwamba mtu hakupaswa wala kutumaini watu hao na vitu vya kimwili, wala kutumaini ushuhuda wao, wala kuwakaribisha kuwa wageni wao, wala kuwa wageni wao, wala hata kununua vitu kutoka kwao. Viongozi wa kidini walisema kwamba kwa binti ya mtu kuolewa na mmoja wa watu hao kungekuwa kama kumfunua kwa hayawani-mwitu akiwa amefungwa na akiwa hoi.