Maelezo ya Chini
a Kwa kuwa Wayahudi wengi waliokuwa nje ya Israeli hawakuwa tena wasomaji wenye ufasaha wa Kiebrania, jumuiya hizo za Kiyahudi kama ile iliyokuwa katika Aleksandria, Misri, upesi ziliona uhitaji wa tafsiri za Biblia katika lugha zao. Ili kusuluhisha uhitaji huo, fasiri ya Septuagint ya Kigiriki ilitayarishwa katika karne ya tatu K.W.K. Fasiri hii baadaye ingekuwa chanzo muhimu sana cha kufanyia mlinganisho.