Maelezo ya Chini
b Karibu na mwaka 760 W.K., kikundi cha Kiyahudi kilichoitwa Wakaraite kilisisitiza kushika zaidi Maandiko. Wakikataa mamlaka ya warabi, “Sheria ya Mdomo,” na Talmud, wao walikuwa na sababu kubwa zaidi ya kulinda mwandiko wa Biblia kitaratibu. Familia fulani katika kikundi hiki zilikuja kuwa wanakili wa Kimasora walio stadi sana.