Maelezo ya Chini
a Kuna zaidi ya mahali 70 katika masimulizi ya Gospeli ambapo Yesu arekodiwa akitumia usemi wa kipekee ili kukazia ukweli wa maneno yake. Mara nyingi angesema “Amina” (“Kwa kweli,” New World Translation) ili kutanguliza sentensi. Neno la Kiebrania linalolingana na hilo lilimaanisha “hakika, kweli.” Yasema The New International Dictionary of New Testament Theology: “Kwa kutanguliza maneno yake kwa amina Yesu aliyataja kuwa hakika na yenye kutegemeka. Alishikamana nayo na kuyafanya yashikamane naye mwenyewe na wasikilizaji wake. Hayo ni wonyesho wa utukufu na mamlaka yake.”