Maelezo ya Chini
a Kotekote katika Maandiko ya Kiebrania, wanaume waliooa na wanawake walioolewa wanarejezewa mara nyingi zaidi kuwa “mume” (Kiebrania, ʼish) na “mke” (Kiebrania, ʼish·shahʹ). Kwa kielelezo, katika Edeni, maneno ambayo Yehova alitumia hayakuwa “mwenye kumiliki” na ‘aliyemilikiwa,’ bali yalikuwa “mume” na “mke.” (Mwanzo 2:24; 3:16, 17) Unabii wa Hosea ulitabiri kwamba baada ya kurudi kutoka uhamishoni, Israeli wangemwita Yehova kwa toba “Mume wangu,” wala si “Mwenye kunimiliki” tena. Hilo huenda likadokeza kwamba neno “mume” lilionyesha wororo zaidi kuliko “mwenye kumiliki.”—Hosea 2:16, NW.