Maelezo ya Chini
a The International Standard Bible Encyclopedia yaeleza hivi: “Wanawake hawakula pamoja na wageni wa kiume, na wanaume walizuiwa wasiongee na wanawake. . . . Mazungumzo pamoja na mwanamke katika mahali pa hadharani lilikuwa jambo la kuchukiza hasa.” Mishnah ya Kiyahudi, ulio mkusanyo wa mafundisho ya kirabi, ilishauri hivi: “Msiongee sana na wanawake. . . . Yeye aongeaye sana na wanawake ajiletea maovu na apuuza funzo la Sheria na mwishowe atarithi Gehena.”—Aboth 1:5.