Maelezo ya Chini
a Vielelezo kutoka kwa Yosefo: Kwenye Mlima Sinai umeme na ngurumo “zilitangaza kwamba Mungu alikuwapo [pa·rou·siʹa] hapo.” Udhihirisho wa kimuujiza katika tabenakulo “ulionyesha kuwapo [pa·rou·siʹa] kwa Mungu.” Kwa kumwonyesha mtumishi wa Elisha yale magari yenye kuzunguka-zunguka, Mungu “alidhihirisha kwa mtumishi wake nguvu [zake] na kuwapo [pa·rou·siʹa] kwake.” Ofisa Mroma Petronius alipojaribu kuwatuliza Wayahudi, Yosefo alidai kwamba ‘Mungu alimwonyesha Petronius kuwapo [pa·rou·siʹa] kwake kwa kutuma mvua. Yosefo hakutumia pa·rou·siʹa kumaanisha kukaribia tu au kuwasili kwa muda. Lilimaanisha kuwapo kwenye kuendelea, hata kusikoonekana. (Kutoka 20:18-21; 25:22; Mambo ya Walawi 16:2; 2 Wafalme 6:15-17)—Linganisha Antiquities of the Jews, Kitabu cha 3, sura ya 5, fungu la 2 [80]; sura ya 8, fungu la 5 [202]; Kitabu cha 9, sura ya 4, fungu la 3 [55]; Kitabu cha 18, sura ya 8, fungu la 6 [284].